NEW POSTS

BREAKING NEWS,WAZIRI, MWIGURU NCHEMBA AMSIMAMISHA MSAJILI WA TAASISI WIZARA YA MABO YA NDANI

Waziri wa mambo ya ndani ya nchi Mhe. Dr MwiguruNchemba amemsimamisha Msajili wa Taasisi wizara ya mabo ya ndani na amefafanua kuhusu nyaraka na matamko yaliyo tolewa na Makanisa kuwa ni mambo ambayo yamepita na hayana tatizo lolote kwa kwa Jeshi la Polisi na Serikali.

Amesema hayo wakati anazungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam na kusema kuwa mambo yanayo sikia katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kuwa ni batili na yapuuzwe. 

Aidha amewataka waumini na viongozi wadini kuendelea na taratibu zao na kusema kuwa serikali haitafumbia macho ambao wanachochea ili kuleta mgawanyiko.

Amewataka wananchi kuacha ushabiki kwani mabo hayo ya naweza kuvuruga amani na umoja wa Taifa.

" Nchi yetu ni moja na tunameweza kuishi siku zote kwa kuheshimiana japo tuna jamii na makabati mengi Tume weza kuishi kama ndugu,"amesema

"Nimefulia hizi nyaraka ambazo zinadaiwa kusambazwa nimeiona zina Anuani tofauti,"amesema

Pia amesimamishwa Msajili wa Taasisi wa mabo ya ndani Marlin Komba,  ili kupisha uchunguzi kujua ukweli  na uhalali wa nyaraka zinazo dawa kusaambaa na ukweli wa  jambo hili kujiridhisha ukweli.

Pamoja na hayo ametoarai kwa wananchi kuhakikisha Wana ilinda amani ya nchi na kuacha kushabikia jambo hilo.

No comments